Meza Huru Podcast By Meza Huru cover art

Meza Huru

Meza Huru

By: Meza Huru
Listen for free

Tanzanian music, from Genesis to currently status told by Stake holders.Meza Huru Music
Episodes
  • Mezani na CHIZAN BRAIN #25
    May 29 2025

    Umeshawahi kujiuliza kwanini mpaka leo kiwanda cha muziki wa Bongo Fleva kina uchache wa Magwiji katika mixing & mastering??? Majina kama Laizer, Mixing killer, Chizan Brain n.k yanatajwa kwa kujirudia kwenye nyimbo za wasanii wengi kwasasababu ni wao tu ndo walioamua kujiongeza kwa kupata knowledge ya ukamilishaji wa project za Audio.Naomba nikukaribishe kwenye ulimwengu wa Chizan Brain, kijana mzaliwa wa Ifakara, Hospitali ya Mtakatifu Francisi, akakulia Tanzania, mpaka alipohamia Kenya kwa Baba yake kumalizia elimu yake sekondari na chuo. Na ndiko aliko anzia safari yake ya muziki kwani Mzee wake pia ni mwanamuziki hodari katika kupiga vyombo takribani vyote, gitaa likiwa ndio chaguo lake la muda mwingi. Akiwa moja wapo wa waanzilishi wa Ukoo flani, akapita studio kadhaa Kenya na muda ulipo fika akahamishia makazi yake nchini Tanzania na kuendelea kukinukisha kwenye tansia ya Muziki wa kizazi kipya. Mezani, Chizan amefunguka kwa kina kuhusu safari yake nzima ya mziki. Karibu ujumuike nasi mezani kumfahamu mkali huyu!!

    Show more Show less
    1 hr and 8 mins
  • Mezani na ASHA BARAKA #24
    Feb 14 2025

    AshaBaraka ni nani? Asha Baraka ni ASHA BARAKA. Unaweza kwenda mbali zaidi ukamuitaMama wa muziki wa dansi Tanzania na usiwe umemzidishia sifa. Asha Barakamwanamichezo kutoka Tabora Girls, Bima hadi kua kocha wa Netball(mpira wapete).

    Lakinileo tunakubaribisha kwenye safari yake kama mwanamke wa kwanza kumiliki bendiya muziki wa dansi Tanzania na mtanzania pekee ambae anaweza sema asilimiakubwa ya wanamuziki wanaofanya mziki wa dansi leo hii wamepita chini ya uongoziwake, iwe ni bendi au chuo cha kufundishia muziki.

    Jeni nani walikua wasanii wa kwanza kabisa Twanga? Banza Stone alikua mahirikiasi gani? Unafahamu Luiza Mbutu alifika fikaje Twanga? Kwanini Ally Chokianaitwa kinanda?

    Yotehaya ameyanyoosha kuweka rekodi sawa. Na ziada si haba. Karibu mezaniumsikilize The Ironylady, Mama, Bibi, Mkurugenzi na Chairman ila sisi tunamuitaNguzo kubwa ya mziki wa dansi Tanzania.

    Show more Show less
    1 hr and 29 mins
  • Mezani na TAJI "MASTER T" LIUNDI #23
    Jan 3 2025

    Kama ulishawahi kuisikia ile story ya mtangazaji wa kwanza kucheza wimbo wa Bongo Fleva kwenye radio. Mtangazaji huyo, leo amepata nafasi ya kutubariki na historia yake. Jinsi alivyochangia muziki huu kuwa kimbilio la vijana wengi sana kama sehemu ya ajira yao.


    Jina lake kamili ni Taji George Liundi au MASTER T kama alivyobatizwa na Charles Hillary. Kuanzia alivyoanza kutangaza Redio One, moja ya vipindi vyake vya awali kabisa cha DJ Show, kabla ya kuwaachia mikoba wakina Mike Mhagama baada ya kuikacha Redio one na kwenda kufanya kazi kwenye media zingine.


    Karibu mezani umfahamu zaidi.

    Show more Show less
    4 hrs and 13 mins
adbl_web_anon_alc_button_suppression_c
No reviews yet