Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama? Podcast Por  arte de portada

Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama?

Hoja za Wahariri Podcast: Nchi bila umeme; ni njama?

Escúchala gratis

Ver detalles del espectáculo
Kupotea kwa umeme nchini Kenya kwa takribani siku tatu kumechochea ghadhabu. Baadhi wanahisi kwamba ni njama ya wafanyakazi fulani wa kampuni za umeme kusababisha hali hiyo maksudi. Kwamba huenda wanalalamikia mageuzi ya usimamizi katika Kenya Power, ama ni kero la wasambazaji wa kawi kulalamikia viwango vipya vya ada za umeme ambavyo ni vya chini, na kuishia wao kupata hasara. Aidha, tunajadili kujiuzulu kwa Mshirikishi wa Utawala, Bonde la Ufa, George Natembeya ili kulenga kiti cha kisiasa. Ali Manzu anawashirikisha wahariri, Charles Otieno na Kennedy Wandera katika kuyajadili masuala haya.
Todavía no hay opiniones